235. Ukae Kwetu Bwana

1.  Ukae kwetu Bwana 

    na rehema yako, 

    Shetani asiweze kutudhuru tena.

 

2.  Ukae kwetu Yesu 

    na Neno la kweli, 

    tupate ukombozi tukilifuata. 


3.  Ukae kwetu nuru

    na mwanga wa mbingu, 

    utuongoze njia iendayo kwako.


4.  Ukae kwetu Bwana

    mwenye enzi yote,

    utupe nguvu nyingi tukutumikie.

 

5.  Ukae kwetu Mponya

    na nguvu yako kuu, 

    adui na dunia wasituharibu.

 

6.  Ukae kwetu Mungu 

    na ukweli wako, 

    tusikuache wewe. Utupeleke juu!


Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima