234. Nifungulie Mlango
1. Nifungulie mlango
niingie Sayuni.
Ndipo nitakapoona
raha na furaha kuu.
Mwokozi anapokaa
Mungu wa utukufu.
2. Nimekuja kwako
Bwana, nakusihi:
Njoo kwangu.
Unapochagua wewe
pana raha ya kweli.
Nakupa moyo wangu
uwe kikao chako.
3. Unisaidie Bwana,
nijiweke tayari,
nyimbo zangu na maombi
yakubalike kwako.
Utakase mwili huu
uwe wako, Bwanangu.
Comments
Post a Comment