233. Mungu Yupo Hapa

1.  Mungu yupo hapa, 

    na tumsujudie,

    tumche tukamtumikie. 

    Yu pamoja nasi, 

    nyamazeni wote 

    Tumwabudu Mungu wetu.

    Wanaolitaja

    Jina lake, njooni,

    tumpeni sadaka.


2.  Mungu yupo hapa,

    anayesifiwa

    na malaika kila siku.

    Wote wanaimba: 

    Mungu Mtakatifu,

    aheshimiwe popote. 

    Ee Mungu sikia 

    tukikuimbia na sisi wadogo.


3.  Twataka kuacha 

    mambo ya dunia

    na uzuri wake wote.

    Mioyo na mapenzi 

    hata nia zetu 

    tunakutolea Bwana.

    Wewe tu, u Mungu, 

    anayestahili sifa za viumbe.


4.  Mwokozi ingia, 

    mioyo yetu yote,

    iwe nyumba yako wewe. 

    Ndiwe Bwana wetu, 

    utusaidie 

    tukupende siku zote.

    Tukiwa wako tu  

    tukae na wewe 

    tukusujudie!


Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima