232. Haleluya, Nakusifu

1.  Haleluya, nakusifu 

    Mungu uliyenipa

    leo tena siku yako, 

    ishindayo nyingine, 

    inanifurahisha 

    moyo wangu kabisa.


2.  Ninaacha masumbuko; 

    leo siku ya Bwana. 

    Ninamtumikia Mungu,

    kwa nguvu zangu zote.

    Leo vyote havifai

    ila kazi ya Mungu.


3.  Ubariki Neno lako

    linapohubiriwa, 

    liingie mioyoni, 

    watu wategemee.

    Nyimbo hata maombi

    yakufikie Mungu.


4.  Unisaidie Bwana 

    nimalize siku hii

    kama nilivyoianza 

    nikikutumikia. 

    Mwisho nione kwako 

    sikukuu ya milele.

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima