231. Mungu Kanilinda Mimi

1. Mungu kanilinda mimi 

   kwa wema mpaka leo. 

   Alinda mwili na roho 

   usiku hata mchana. 

   Aniongoza kila saa, 

   apenda kunibariki

   na kunisaidia.


2. Ninakushukuru Mungu 

   sababu ya rehema,

   uliyonifanyizia 

   Bwanangu siku zote.

   Ninakumbuka daima

   mambo unitendeayo,

   ukanisaidia.


3. Uzidi kunibariki,

   kwa wema wako Bwana.

   Nisaidie kila saa

   na mahali popote. 

   Nimshike Yesu Mwokozi, 

   hata na siku ya kufa 

   nipate mwisho mwema. 

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima