229. Usiku Uingiapo

1.  Usiku uingiapo,

    umwaze Mungu Mkuu,

    aendeshaye dunia

    kwa mwendo mtulivu.


2.  Kwa nini wahangaika 

    usiku na mchana? 

    Umtwishe huzuni yako 

    aliyekuumba.


3.  Kwake haujapunguka 

    uwezo na msaada. 

    Atayatimiza yote 

    aliyoyaanza.


4.  Ukamwachie kutenda

    atakalo kwako!

    Kwa hiyo ulale raha 

    na kufurahiwa. 

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima